International Tennis Federation (ITF) yaibeba tenisi ya Tanzania


Viongozi wa TTA wakiongea na waandishi
Shirikisho la Tenisi la Kimataifa (ITF) limetoa nafasi moja ya upendeleo kwa mchezaji wa Tanzania kushiriki kwenye mashindano ya Tenisi ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 18 yaliyopangwa kufanyika mapema Machi katika nchi mbili tofauti.

Awali Tanzania ilipitisha wachezaji wanne waliofuzu kushiriki kwenye mashindano hayo ambayo yatafanyika jijini Nairobi, Kenya kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 16 na Cassablanca, Morocco kwa wachezaji chini ya miaka 18.

Kwa mujibu wa kocha wa timu ya taifa ya vijana, Kiango Kipingu, chama cha Tenisi Tanzania (TTA) kimepewa nafasi nyingine moja kwenye michuano hiyo ambayo ITF imesema itachagua yenyewe mchezaji huyo ambaye itamghariamia kwa kila kitu.

“Kutokana na motisha hiyo ya ITF sasa Tanzania itawakilishwa na wachezaji watano ambao wanne kati yao walifikia viwango vya kushiriki mashindano ya Afrika baada ya kufanya vizuri kwenye yale ya Afrika Mashariki na kati hivi karibuni jijini Dar es Salaam,” alisema Kipingu.

Alisema wachezaji waliofikia viwango, watatu wako Nairobi ambako huko wameweka kambi na watashiriki kwenye mashindano ya dunia ya vijana chini ya miaka 18 yanayoendelea kwa wiki tatu jijini humo ambayo yatakuwa sehemu ya maandalizi yao.

“Tumaini Mishuko, Emmanuel Malya na Omary Sule wako Nairobi ambapo baada ya mashindano ya dunia watakwenda Morocco kule watashiriki mashindano mengine ambayo yatakuwa sehemu ya maandalizi yao,” alisema.

Chanzo: Mwananchi

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga